Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 50 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 416 2021-06-14

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa barabara kutoka Mnivata hadi Masasi kupitia Newala kwa kiwango cha lami utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Nanyamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara Mnivata, Newala, Masasi yenye urefu wa kilometa 160 ni sehemu ya barabara ya Mtwara, Nanyamba, Tandahimba, Newala hadi Masasi yenye urefu wa kilometa 210.

Mheshimiwa Naibu Spika, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Mtwara, Nanyamba, Tandahimba, Newala hadi Masasi yenye urefu wa kilometa 210 umekamilika. Ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha ambapo awamu ya kwanza ya sehemu ya Mtwara hadi Mnivata yenye urefu wa kilometa 50 imekamilika.

Aidha, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imetenga shilingi milioni 3,000 kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu ya Mnivata, Newala, Masasi yenye urefu wa kilometa 160.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia kwa Wakala wa Barabara (TANROADS) inaendelea kuifanyika matengenezo mbalimbali barabara hii ili kuhakikisha kuwa inapitika majira yote ya mwaka ambapo katika mwaka wa fedha 2021/2022 jumla ya Shilingi Milioni 1,017.33 zimetengwa. Ahsante