Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 50 Water and Irrigation Wizara ya Maji 414 2021-06-14

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza upembuzi yakinifu na ujenzi wa miundombinu ya maji katika Ziwa Madunga ili kutatua tatizo sugu la maji katika Kata ambazo hazina maji Jimbo la Babati Vijijini?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sillo Daniel Baran, Mbunge wa Babati Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa Babati Vijijini ni asilimia 74. Kwa lengo la kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama na yenye kutosheleza kwa wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Babati, Serikali inaendelea na utafiti wa ubora na uwingi wa maji katika chanzo cha Ziwa Madunga. Utafiti huo unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni, 2021 na usanifu wa miundombinu ya maji utakamilika katika robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/2022.