Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 50 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 413 2021-06-14

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha mpango wa uvunaji wa mikoko kwa wananchi wanaoishi maeneo ya Delta wanaotegemea zao hilo kuendesha shughuli zao za kimaisha?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba ama napenda kujibu swali la Mheshimiwa Twaha Ally Mpembenwe, Mbunge wa Kibiti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, misitu ya mikoko ina umuhimu mkubwa katika nyanja za kiuchumi na kimazingira, kutokana na kuvamiwa kwa misitu hii kwa kufanya shughuli zisizokubalika kiuhifadhi kama vile kilimo, ufugaji utayarishaji wa chumvi, Serikali ilisimamisha uvunaji wa mikoko yote kote nchini ili kutoa fursa ya kuweka mipango na mikakati ya matumizi endelevu. Hivyo, Wizara inaandaa mpango na mwongozo wa usimamizi wa matumizi endelevu ya misitu ya mikoko utakaotoa utaratibu wa uvunaji. Mipango na miongozo hiyo ipo katika hatua za mwisho za maandalizi na inatarajiwa kukamilika robo ya kwanza ya mwaka 2021/2022 na baada ya kukamilika utaanza kutumika.