Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 50 Investment and Empowerment Ofisi ya Rais: Mipango na Uwekezaji 410 2021-06-14

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:

Je, mpaka sasa ni wawekezaji wangapi wamemilikishwa ardhi na kupata Hati kupitia Kituo cha Uwekezaji TIC?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU, UWEKEZAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, wawekezaji wa kigeni wanamiliki ardhi kwa ajili ya uwekezaji kupitia Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kwa utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi Na.4 ya mwaka 1999. Kifungu cha 20 cha Sheria hiyo kinaelekeza kwamba, Kamishna wa Ardhi atatoa hati ya umiliki wa ardhi (Certificate of Right of Occupancy) kwa jina la Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kwa ajili ya uwekezaji endapo uwekezaji huo unafanywa na mwekezaji wa kigeni. Kwa kutumia hati hiyo, TIC hutoa Hati ya Umiliki Isiyo Asili (Derivative Right) kwa mwekezaji wa kigeni aliyewasilisha maombi ya ardhi kwa ajili ya uwekezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya mwekezaji kupewa Hati ya Umiliki Isiyo Asili na TIC, hati hiyo inasajiliwa na Msajili wa Hati (Registrar of Titles) ambaye anatoa hati ya umiliki wa ardhi hiyo (Derivative Title) kwa jina la mwekezaji wa kigeni kulingana na masharti ya uwekezaji husika kama yalivyoainishwa kwenye mkataba wake na TIC.

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia utaratibu huo, tangu mwaka 1999 hadi mwezi Mei, mwaka huu, Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimewezesha upatikanaji wa Hati za Umiliki Zisizo Asili (Derivative Rights) 401 kwa wawekezaji wa kigeni.