Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 49 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 409 2021-06-10

Name

Ali Hassan Omar King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Jang'ombe

Primary Question

MHE. ALI HASSAN OMAR KING aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kufungua Ofisi Ndogo ya Hazina Zanzibar kama ilivyo kwa taasisi nyingine za Muungano ili kurahisisha huduma kwa wastaafu wa Jamhuri ya Muungano wanaoishi Zanzibar?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ali Hassan Omar King, Mbunge wa Jang’ombe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, huduma za malipo ya mafao ya wastaafu wanaolipwa na Wizara ya Fedha na Mipango hufanyika kupitia Ofisi za Hazina Makao Makuu, Dodoma. Aidha, Ofisi za Hazina Ndogo zilizopo katika Mikoa ya Tanzania Bara hutumika kwa ajili ya kukusanya hoja za wastaafu na kuziwasilisha Hazina Makao Makuu, Dodoma.

Mheshimiwa Spika, kwa wastaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanaoishi Zanzibar, Wizara ya Fedha na Mipango ya Serikali ya Muungano wa Tanzania mara zote imekuwa ikifanya kazi kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa ajili ya kupokea hoja za madai ya wastaafu hao na kuziwasilisha Hazina Makao Makuu, Dodoma kwa ajili ya taratibu za malipo.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Fedha na Mipango ya Serikali ya Muungano wa Tanzania itaimarisha ushirikiano na Wizara ya Fedha na Mipango ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika kuwahudumia wastaafu wa Jamhuri ya Muungano wanaoishi Zanzibar kama ambavyo hushirikiana na Ofisi za Hazina Ndogo zilizopo Tanzania Bara.