Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 48 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 403 2021-06-09

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SYLIVIA F. SIGULA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha wavuvi wa Ziwa Tanganyika wavue kisasa ili kupata kipato zaidi na kutoa ajira kwa vijana?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiaw Waziri wa Mifugo na Uvuvi naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Sylivia Francis Sigula, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika juhudi za kusaidia na kuwezesha wavuvi wadogo kuvua kisasa, Serikali imerahisisha utaratibu wa kupata zana za kisasa za uvuvi. Serikali imefuta Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwenye vifaa vingi vya uvuvi ikiwemo engine za kupachika, nyuzi za kushonea nyavu, nyavu za uvuvi na vifungashio kupitia Sheria ya Fedha ya mwaka 2011 na Sheria ya Mamlaka ya Mapato ya mwaka
2014 ili kuwasaidia wavuvi kupata zana za uvuvi kwa bei nafuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Vilevile, Serikali inaendelea kuweka mazingira mazuri ili wavuvi wapate mikopo ya masharti na riba nafuu kutoka katika Benki ya Maendeleo ya Kilimo kwa maana TIB. Aidha, Wizara kupitia Dawati la Sekta Binafsi imeviunganisha vyama vya ushirika vya wavuvi na taasisi za fedha ambapo mikopo iliyoombwa na kupitishwa ni shilingi bilioni 2.6 na mikopo iliyotolewa ni shilingi milioni 560.7. Pia Wizara imehamasisha Benki ya Posta kuanzisha na kuzindua Akaunti ya Wavuvi kwa ajili ya mikopo na bima mahususi kwa wavuvi hususan wavuvi wadogo.