Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 48 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 398 2021-06-09

Name

Rashid Abdalla Rashid

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiwani

Primary Question

MHE. RASHID ABDALLA RASHID aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Jimbo la Kiwani ili kuepusha wananchi kufuata huduma za Polisi masafa marefu?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdalla Rashid, Mbunge wa Kiwani kutoka Mkoa wa Kusini Pemba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua hitajio la Kituo cha Polisi eneo la Kiwani na kwa sasa wananchi wa Kiwani wanapata huduma ya polisi kutoka katika Kituo cha Polisi Kengeja ambacho kipo umbali wa kilometa tano tokea Kiwani Central.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka sasa sehemu ya Kiwani hakuna eneo lililotengwa na Halmashauri ya Wilaya ya Mkoani kwa ajili ya kujenga Kituo cha Polisi na nyumba za makazi ya askari.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu ni kwamba Mheshimiwa Mbunge kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya pamoja na wananchi ili kutoa eneo kwa Jeshi la Polisi litakalotosha kwa mahitaji ya ujenzi wa Kituo cha Polisi pamoja na makazi ya askari, ili Jeshi la Polisi liweze kutoa huduma karibu na wananchi katika eneo hilo la Kiwani, nashukuru.