Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 47 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 394 2021-06-08

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa barabara ya Mianzini, Sambasha, Ngaramtoni hadi Hospitali ya Selari kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Noah Lemburis Ole Saputu, Mbunge wa Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, aliagiza barabara ya Mianzini – Sambasha – Ngaramtoni hadi Hospitali ya Selari yenye urefu wa kilometa 18 kupandishwa hadhi ili isimamiwe na Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) na aliagiza ijengwe kwa kiwango cha lami. Awali barabara hii ilikuwa inasimamiwa na Halmashauri za Arusha DC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia agizo la Mheshimiwa Rais, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) ilifanya usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami pamoja na utayarishaji wa makabrasha ya zabuni kazi ambayo ilikamilika mwaka 2019. Zabuni za ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami kwa kilometa zote 18 zimetangazwa tarehe 17 Mei, 2021.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi za ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami zitaanza mara baada ya tathmini ya zabuni kukamilika na mkandarasi kupatikana. Katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 jumla ya shilingi bilioni 2.5 zimetengwa kwa ajili ya mradi huu. Ahsante.