Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 47 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 392 2021-06-08

Name

Salim Alaudin Hasham

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. SALIM A. HASHAM aliuliza:-

Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Ifakara – Mahenge utaanza kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Alaudin Hasham Salim, Mbunge wa Ulanga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Ifakara –Mahenge ni sehemu ya Barabara Kuu ya Mikumi, Kidatu, Ifakara, Lupiro, Mahenge/Malinyi, Kilosa kwa Mpepo, Londo hadi Lumecha yenye urefu wa kilometa 547 ambayo inaunganisha Mikoa ya Ruvuma na Morogoro. Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii ilikamilika mwaka 2018 kwa lengo la kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi sasa ujenzi wa Daraja la Magufuli lenye urefu wa mita 384 pamoja na barabara unganishi yenye urefu wa kilometa 9.142 umekamilika. Ujenzi wa sehemu ya Ifakara – Lupiro – Mahenge utaanza kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati juhudi za kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami zikiendelea, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) itaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara husika ili ipitike majira yote ya mwaka. Ahsante.