Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 47 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 391 2021-06-08

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KACHAUKA K.n.y. MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza:-

Je, Serikali iko tayari kuunga mkono juhudi za wananchi wa Kata ya Makata - Liwale ambao wameanzisha ujenzi wa Chuo cha VETA na madarasa mawili yamekamilika?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kachauka, Mbunge Liwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua jitihada zinazofanywa na wananchi za kuona umuhimu wa kuwa na Chuo cha Ufundi Stadi katika maeneo yao wakiwemo wananchi wa Kata ya Makata - Liwale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, azma ya Serikali ni kujenga Chuo cha Ufundi Stadi katika kila Wilaya nchini. Katika kutimiza azma hiyo, Serikali inaendelea na ujenzi wa Vyuo vya Ufundi Stadi katika Wilaya 29 nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Serikali inaendelea na mpango huu kwa awamu, nashauri wananchi wa Kata ya Makata waendelee na juhudi hizo wakati Serikali inaendelea kutafuta fedha. Aidha, niombe uongozi wa Wilaya ya Liwale uwasiliane na uongozi wa VETA kuweza kuona namna ya kupata msaada wa kitaalam kuhusu ujenzi wa majengo ya Vyuo vya Ufundi Stadi. Ahsante.