Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 46 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 386 2021-06-07

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakuja na Mpango Madhubuti wa kuitumia Bahari kwa Programu za Uvuvi wa Bahari Kuu na michezo ya bahari ili kutengeneza ajira kwa Vijana wa Jimbo la Kawe, hasa ikizingatiwa nusu ya Jimbo hilo lipo Mwambao wa Bahari ya Hindi?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Askofu Josephat Mathias Gwajima, Mbunge wa Kawe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na juhudi za kuimarisha uvuvi wa bahari kuu kwa kufufua Shirika la Uvuvi Tanzania, TAFICO ili kuiwezesha nchi kunufaika na rasilimali za uvuvi. Hususani zile zilizopo katika ukanda wa uchumi wa bahari kuu na bahari ya ndani. Hadi sasa Serikali ina mpango wa kununua meli tano za uvuvi, ambazo zitavua katika maji ya Kitaifa, Bahari kuu pamoja na kutoa leseni kwa meli kubwa zinazomilikiwa na sekta binafsi.

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango wa kujenga bandari ya uvuvi katika ukanda wa pwani ya Bahari ya Hindi. Ambapo uwepo wa bandari hiyo, utawezesha meli za uvuvi zinazovua katika ukanda wa uchumi wa bahari ya Tanzania na bahari kuu kutia nanga, kushusha mazao ya uvuvi na kupata huduma mbalimbali, zikiwemo mafuta na chakula ambapo meli hizo zitachangia kutoa ajira kwa wananchi wakiwemo wa Jimbo la Kawe.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuboresha mazingira na usalama katika fukwe na visiwa vya Bahari ya Hindi, ili kuwavutia wawekezaji kuwekeza katika shughuli mbalimbali za michezo katika fukwe na visiwa hivyo.