Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 46 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 385 2021-06-07

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza:-

Je, ni lini upanuzi wa Kiwanda cha Sukari cha Ilovo utakamilika, na kwa kiasi gani upanuzi huo utaenda sambamba na kuondoa kero ya Mizani na Vipimo vya Sucrose kwa wakulima wa Miwa?

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Answer

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dennis Lazaro Londo, Mbunge wa Jimbo la Mikumi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kiwanda cha Sukari cha Kilombero kinaendeshwa na Kilombero Sugar Company Limited, Kampuni hii inamilikiwa kwa ubia kati ya Kampuni ya Ilovo Sugar Africa yenye asilimia 75 na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yenye asilimia 25 katika hisa hizo. Katika kutekeleza sera ya Serikali ya kujitosheleza kwa mahitaji ya sukari nchini ifikapo mwaka 2025, Kampuni ya Kilombero Sugar itatekeleza mradi wa upanuzi wa Kiwanda cha Sukari cha Kilombero kwa gharama ya shilingi bilioni 571.6.

Mheshimiwa Spika, matokeo tunatarajia mradi huu ni kuwa na Kiwanda cha kisasa, ambacho kitakuwa kikubwa mara nne kuliko cha sasa, kuongeza uzalishaji wa sukari mara mbili kutoka tani 127,000 za sasa hadi tani 271,000 kwa mwaka. Kuongeza mara tatu matumizi ya miwa kutoka kwa wakulima wadogo kutoka tani 600,000 hadi tani milioni 1.7 na kuongeza zaidi ya mara tatu idadi ya wakulima wanaouza miwa kutoka wakulima 7,500 hadi 15,000 mpaka 16,000. Mazungumzo kati ya wabia kuhusu mradi huu yamekamilika na utekelezaji wake utaanza mwezi Juni, ambao ni mwezi huu na unatarajiwa ukamilike mwezi Julai mwaka 2023.

Mheshimiwa Spika, kuhusu sehemu yake ya pili ya swali, Serikali inatambua changamoto ya kero ya mizani na upimaji wa ubora wa miwa kwa wakulima wa miwa huko Kilombero. Katika kutatua changamoto hii, Serikali inalenga kuwa na mizani huru tofauti na ya sasa, ili tuwe na wapimaji huru na nimeshawaelekeza Work and Measures Agency wafanye utafiti kuona uwezekano wa wao wenyewe kupima, badala ya kupima na Kiwanda cha Kilombero. Ahsante sana. (Makofi)