Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 46 Water and Irrigation Wizara ya Maji 384 2021-06-07

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Primary Question

MHE. JUMANNE A. SAGINI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Kata za Bwiregi, Nyamimange, Buswahili na Sirorisimba zinapata maji ya Ziwa Victoria kwa kuwa Mradi wa Maji wa Mgango – Kyabakari – Butiama hautazifikia?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jumanne Abdallah Sagini, Mbunge wa Butiama, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha Kata za Bwiregi, Nyamimange, Buswahili na Sirorisimba zinapata huduma ya majisafi na salama, Serikali katika mwaka wa fedha 2020/ 2021 imekarabati miradi ya maji katika Vijiji vya Kamgendi, Masurura, Kongoto, Kitaramanka na Rwasereta.

Mheshimiwa Spika, kazi zilizofanyika ni ukarabati wa vituo 42 vya kuchotea maji, kukarabati bomba kuu na bomba la kusambaza maji kilometa 18.5. Ukarabati wa nyumba ya mitambo ya kusukuma maji, ununuzi na ufungaji wa pampu, ufungaji wa umeme wa TANESCO katika Kijiji cha Masurura. Ukarabati wa miradi hii umekamilika ambapo wananchi wapatao 12,220 wananufaika na huduma ya maji kuanzia mwezi Machi, 2021.

Mheshimiwa Spika, katika kuendelea kuboresha huduma ya maji katika Kata za Nyamimange, Buswahili, Bwiregi na Sirorisimba, Serikali imepanga kutekeleza miradi mbalimbali, ikiwemo ujenzi wa matenki ya kuhifadhi maji yenye lita za ujazo 150,000, 90,000. Ujenzi wa vituo vya kuchotea maji 30, ulazaji wa bomba kuu na bomba la kusambaza maji jumla ya urefu wa kilometa 26. Ujenzi wa nyumba za mashine, ujenzi wa nyumba za jumuiya za watumia maji na ufungaji wa mfumo wa umeme.

Mheshimiwa Spika, miradi hii ikikamilika itanufaisha wakazi wapatao 7,024 wa kata hizo. Katika mpango wa muda mrefu, huduma ya maji itaboreshwa katika Kata ya Bwiregi, Nyamimange, Buswahili na Sirorisimba na maeneo mengine kupitia upanuzi wa mradi wa maji Mugango, Kabari na Butiama.