Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 46 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 378 2021-06-07

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza:-

Je, kwa nini wazazi wanachangishwa michango ya kuchangia elimu wakati Serikali inasema Elimu kwa Shule ya Msingi na Sekondari ni bure?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Waraka wa Elimu Na.5 wa mwaka 2015 iliamua kutoa elimumsingi bila malipo kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha nne. Uamuzi huo ulijielekeza katika kutekeleza Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 ambayo ina lengo la kuhakikisha watoto wote wa Kitanzania wenye rika la elimumsingi wanapata elimu bila kikwazo chochote ikiwemo ada au michango. Aidha, Serikali ilitoa Waraka wa Elimu Na.3 wa mwaka 2016 kuhusu utekelezaji wa elimumsingi bila malipo. Waraka huu unafafanua maana ya elimumsingi na kuainisha majukumu ya kila kundi linalohusika katika utoaji wa elimumsingi bila malipo na kuweka utaratibu wa utekelezaji wake.

Mheshimiwa Spika, majukumu ya jamii na wananchi kuhusu michango yamebainishwa kwenye Waraka wa Elimu Na.3 wa mwaka 2016. Waraka unaeleza kuwa Kamati za Shule au Bodi za Shule zitashirikisha jamii katika maazimio na maamuzi ya masuala mbalimbali yanayohusu maslahi na maendeleo ya shule hususan uchangiaji wa hiari na kuwasilisha maamuzi hayo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ili kupata kibali. Hivyo, uchangiaji katika elimu unaoruhusiwa ni wa hiari na hauhusishi wanafunzi kuzuiwa kuhudhuria masomo.