Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 46 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 377 2021-06-07

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaongezea TARURA fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara kwa kuzingatia ukuaji wa kasi wa Miji na Halmashauri zetu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jesca Jonathan Msambatavangu, Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2021/ 2022, Serikali imeitengea TARURA shilingi bilioni 400 kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya miundombinu ya barabara na madaraja. Bajeti hiyo ni ongezeko la shilingi bilioni 124.97 kutoka bajeti ya shilingi bilioni 275.03 iliyotengwa kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya miundombinu ya barabara na madaraja katika Mwaka wa Fedha 2020/2021.

Mheshimiwa Spika, sambamba na kuipatia TARURA fedha kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya miundombinu ya barabara na madaraja, Serikali imeendelea na ujenzi wa miundombinu katika miji inayokua kupitia mipango mbalimbali kama vile Mpango wa Uboreshaji wa Miji Mikakati ambayo ilihusisha Majiji na Manispaa kupitia Mradi wa Uendelezaji Miji ya Kimkakati (TSCP), Programu ya Kuimarisha Halmashauri za Miji 18 (ULGSP) ikiwemo Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na Mradi wa Uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP).

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na maandalizi ya Mradi wa Kuboresha Miundombinu ya Mijini (TACTIC) na Mradi wa Uendelezaji wa Miundombinu ya Mkoa wa Dar es Salaam, awamu ya pili (DMDP II) kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ikiwemo barabara, madaraja, stendi za mabasi na masoko.