Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 43 Water and Irrigation Wizara ya Maji 365 2021-06-03

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga Mradi wa Maji ambao ulishafanyiwa upembuzi yakinifu kwa Wananchi wa Vijiji vya Nkome, Mchangani, Katome, Nyamboge, Nzera na Rwezera?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Kasheku Musukuma, Mbunge wa Geita Vijiji, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi wa maji ambao utahudumia Vijiji vya Nkome, Mchangani, Katome, Nyamboge, Nzera na Rwezera utaanza katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2021/2022. Kwa mwaka wa fedha 2021/2022 mradi huo umetengewa kiasi cha shilingi bilioni 1 kwa ajili ya kuanza kazi ambazo itahusisha ujenzi wa chanzo cha maji na kituo cha kusukuma maji kwa maana ya booster; ulazaji wa bomba zaidi ya kilometa 70, ujenzi wa matanki ya kuhifadhia maji pamoja na ujenzi wa vituo vya kuchotea maji. Aidha, mradi huo umepangwa kunufaisha Vijiji vingine vya Mnyala, Ihumilo, Nyambaya, Nyakazeze, Itale, Njingami, Lukaya, Chelameno, Bugando, Igate, Bweya, Idosero na Nyarubanga.