Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 43 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 361 2021-06-03

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza:-

Je, ni lini barabara ya Kisamba – Sayaka hadi Salama inayounganisha Mkoa wa Mwanza na Simiyu itaanza kuhudumiwa na TANROADS?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Boniventura Destery Kiswaga, Mbunge wa Magu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Kisamba – Sayaka hadi Salama ni barabara ya Wilaya inayohudumiwa na Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA).

Mheshimiwa Spika, ili barabara yoyote iweze kuhudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) zipo taratibu ambazo lazima zifuatwe ikiwa ni pamoja na maombi ya kupandishwa hadhi ya kuwa barabara kuu ama ya mkoa kuwasilishwa kwenye mamlaka zinazohusika kwa kuzingatia utaratibu ulioainishwa kwenye Sheria ya Barabara ya mwaka 2007 na Kanuni zake za mwaka 2009 ambayo imeainisha pia vigezo vinavyohitajika katika kupandisha hadhi barabara. Ahsante.