Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 42 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 360 2021-06-02

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:-

Sehemu kubwa ya maeneo ya Kilimo cha Mpunga Malinyi imemegwa na Mamlaka ya Wanyamapori (TAWA) kwa Mipaka mipya iliyowekwa Mwaka 2017 bila maridhiano na Wananchi wa sehemu ya bonde la Kilombero. Je, Serikali haioni kuwa ni vema kufanya upya mapitio shirikishi kwenye mipaka ya eneo la Hifadhi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Antipas Zeno Mgungusi, Mbunge wa Malinyi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, eneo la Bonde la Kilombero ni sehemu ya ardhioevu yenye umuhimu kitaifa na kimataifa kutokana na kuhifadhi bioanuai mbalimbali na zilizo adimu duniani kama vile mnyama aina ya sheshe. Aidha, Bonde hilo huchangia takriban asilimia 62.5 ya maji yote ya Mto Rufiji na hivyo kuwa chanzo muhimu cha maji kwa mradi wa kufua umeme wa Julius Nyerere.

Mheshimiwa Spika, uwekaji wa mipaka wa Bonde la Kilombero ulizingatia mfumo halisi wa kiikolojia wa Bonde hilo, ili uweze kukidhi matarajio ya uhifadhi wa ardhioevu. Hivyo basi, Pori Tengefu Kilombero lilianzishwa mwaka 1952 kwa GN. Na. 107/1952 na halijawahi kubadilishwa mipaka yake. Naomba kuwasilisha.