Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 42 Water and Irrigation Wizara ya Maji 358 2021-06-02

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza:-

Jimbo la Kibaha Mjini bado lina changamoto kubwa ya maji katika maeneo ya Kata za Mbwawa na Pangani; na Mradi wa Ujenzi wa matanki ya maji unakwenda kwa kusuasua. Je, ni lini Mradi huo utakamilika ili Wananchi wa Kibaha Mjini waondokane na adha ya maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Silvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2020/21, Serikali imekamilisha utekelezaji wa mradi wa maji ambao ulihusisha ulazaji wa bomba kuu pamoja na mabomba kwa ajili ya kutawanya maji kwa wananchi yenye urefu wa kilomita 27. Wananchi wapatao 6,500 wa Kata ya Mbwawa wananufaika na huduma ya maji tangu mwezi Aprili, 2021. Kwa upande wa Kata ya Pangani usanifu kwa ajili ya ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji lita millioni 6 umekamilika.

Mheshimiwa Spika, mwaka wa fedha 2021/2022, jitihada za kuboresha huduma ya maji katika maeneo ya Kibaha Mjini zinaendelea na kazi ya ujenzi wa tenki kubwa utaanza na ulazaji wa bomba kuu urefu wa kilomita tano utaanza katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2021/ 2022. Mradi huu utanufaisha wananchi wa Kata ya Pangani, pamoja na eneo la Viwanda la Kibaha Mjini (TAMCO).