Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 42 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 353 2021-06-02

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza:-

(a) Je, ni lini Serikali itawalipa wananchi wanaodai miche ya mikorosho deni ambalo ni la muda mrefu tangu mwaka 2017?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ally Mchungahela Mbunge wa jimbo la Lulindi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika msimu wa mwaka 2017/ 2018 Serikali kupitia Bodi ya Korosho iliingia mikataba na wazalisahji wa miche 678 ili kuzalisha miche 13,661,433 ya korosho yenye thamani ya shilingi 5,317,107,679. Aidha, jumla ya miche 12,298,000 sawa na asilimia 92 imesambazwa kwa wakulima katika Mikoa ya Mtwara, Lindi, Ruvuma, Pwani, Tanga, Singida, Tabora, Dodoma, Kilimanjaro, Morogoro, Njombe, Mbeya, Iringa na Songwe.

Mheshimiwa Spika, malipo kwa wazalishaji hao yamechelewa kutokana na zoezi la uhakiki kuchukua muda ili kujiridhisha kabla ya kufanya malipo hayo. Kutokana na uhakiki uliofanywa katika awamu ya kwanza na timu ya wataalamu kutoka Serikalini jumla wazalishaji miche 382 waliozalisha miche milioni tano yenye thamani ya shilingi bilioni 2.3 wameshalipwa.

Aidha, kupitia uhakiki wa awamu ya pili uliofanyika mwezi Agosti hadi Oktoba 2020, ulibaini kuwa jumla ya miche milioni 5.8 yenye thamani ya shilingi bilioni 2.660 ilihakikiwa na bado kulipwa. Aidha, Serikali inakamilisha utaratibu wa malipo kwa wazalishaji hao wa miche na watalipwa.