Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 40 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 334 2021-05-31

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kupeleka watumishi wa Idara ya Afya katika Jimbo la Kilwa Kaskazini ambalo lina uhaba mkubwa wa watumishi kiasi cha kufanya baadhi ya zahanati kutoa huduma duni na nyingine kuchelewa kufunguliwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kaskazini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa ina jumla ya vituo vya kutolea huduma za afya 60 zikiwemo hospitali mbili, vituo vya afya vitano na zahanati 53. Katika kipindi cha kuanzia mwaka 2017 hadi Desemba, 2020, Serikali imeajiri na kuwapanga watumishi 108 wa kada mbalimbali za afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa. Aidha, mwezi Mei, 2021 Ofisi ya Rais-TAMISEMI imetangaza nafasi 2,726 za ajira za kada mbalimbali za afya. Watumishi hao watapangwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kote nchini kwa kutoa kipaumbele kwenye vituo vya kutolea huduma za afya vyenye upungufu mkubwa wa watumishi ikiwemo baadhi ya vituo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa.

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kuendelea kuajiri watumishi wa kada mbalimbali za afya na kuwapangia katika vituo Wilayani Kilwa na kote nchini kwa ujumla, ahsante sana.