Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 41 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 350 2021-06-01

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA aliuliza:-

(a) Je, ni taasisi ngapi zilizo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango hadi sasa hazina Bodi au Bodi zake zimemaliza muda wake?

(b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha benki ya waliopekuliwa ili muda wowote uteuzi ufanyike haraka kusaidia Taasisi hizo kwenda na kasi ya Mheshimiwa Rais kwani kwa sasa upekuzi imekuwa kisingizio cha kuchelewesha uteuzi?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jerry William Silaa, Mbunge wa Ukonga lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Fedha na Mipango ina jumla ya Taasisi 28 ambazo inazisimamia na kati ya hizo Taasisi tisa Bodi zake zimemaliza muda wake na mapendekezo ya majina kwa ajili ya kujaza nafasi za Wenyeviti na Wajumbe wa Bodi hizo yamewasilishwa kwenye Mamlaka za Upekuzi.

Mheshimiwa Spika, upekuzi kwa ajili ya kujaza nafasi mbalimbali hufanyika kwa wakati husika kutokana na ukweli kwamba utendaji na mienendo ya maafisa hubadilika kutoka wakati mmoja hadi mwingine. Hivyo, siyo sahihi kuwa na kanzidata ya upekuzi (benki ya waliopekuliwa) ili kurahisisha mchakato wa upekuzi kwa kuwa utendaji na mienendo ya maafisa hubadilika kuendana na wakati husika.