Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 41 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 343 2021-06-01

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati barabara zilizoharibika hasa barabara za vijijini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua adha kubwa inayotokana na kuharibika kwa miundombinu ya barabara uliosababishwa na mvua nyingi zilizonyesha msimu wa mwaka 2019/2020 na msimu wa mwaka 2020/2021.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeongeza bajeti ya matengenezo ya barabara ya Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kutoka shilingi bilioni 275.03 iliyotengwa katika mwaka wa fedha 2020/2021 hadi shilingi bilioni 400 iliyotengwa katika mwaka wa fedha 2021/2022 ambalo ni ongezeko la Shilingi bilioni 124.97 sawa na aslimia 45.4. Ongezeko hili litaiwezesha TARURA kufanya matengenezo ya miundombinu ilyoharibika kwa awamu.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti ya ujenzi na matengenezo ya barabara kadri ya upatikanaji wa fedha, ahsante.