Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 36 Works, Transport and Communication Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 302 2021-05-25

Name

Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Primary Question

MHE. KATANI A. KATANI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka Mawasiliano ya Simu yenye usikivu katika Kata ya Litehu, Ngunja na Mkwiti Wilayani Tandahimba?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari naomba kujibu swali la Mheshimiwa Katani Ahmed Katani Mbunge wa Tandahimba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote unatekeleza miradi saba katika kata sita za Jimbo la Tandahimba kupitia Mradi wa Awamu ya nne na tano . Miradi hiyo inatekelezwa katika Kata za Chaume, Mdimba Mnyoma, Mkoreha katika Kijiji cha Chikongo, Ngunja. Kuna miradi miwili mmoja uko Kijiji cha Ngunja na mwingine Namindondi Juu, lakini katika Kata ya Mihambwe, na Namikupa utekelezaji wa mradi uliopo katika hizo Kata unaendelea.

Mheshimiwa Spika, Pamoja na jitihada hizo za Serikali, bado kuna maeneo mengi ya Jimbo la Tandahimba ambayo yana changamoto za mawasiliano. Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano imevifanyia tathmini vijiji vya Kata za Litehu, Ngunja na Mkwiti katika Jimbo hilo.

Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha kwamba zinaingizwa katikazabuni ya mradi wa mipakani na kanda maalumu ya Kanda Maaalum awamu ya sita yaani Border and Special Zone Phase six Mradi huu unatarajiwa kutangazwa kabla ya kuisha kwa mwaka wa fedha 2020/2021.