Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 36 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 300 2021-05-25

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L.S. MOLLEL aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itawalipa fidia ya kupisha njia kubwa ya umeme wananchi wa Vijiji vya Lengijape, Ilkurot na Olkejulenderit katika Jimbo la Arumeru Magharibi?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Noah Lemburis Saputu Mollel, Mbunge wa Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Shirika la Umeme TANESCO inaendelea kukamilisha ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoti 400 kutoka Singida hadi Namanga. Lengo kuu la mradi huu ni kuimarisha upatikanaji wa umeme katika Gridi ya Taifa.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TANESCO imeshalipa fidia kwa wananchi wote jumla ya shilingi bilioni 52.67 zikiwa ni fidia kwa wananchi 4,526 katika mikoa yote mitatu iliyoguswa na mradi huu wakiwemo wananchi wa Vijiji vya Lengijape, llkurot na Olkejulenderit katika Jimbo la Arumeru Magharibi. Aidha, Serikali kupitia TANESCO imeshalipa fidia kwa taasisi zilizopo katika vijiji vyote vya Wilaya za Singida Vijijini, Hanang, Babati na Longido.

Mheshimiwa Spika, maandalizi ya ulipaji wa fidia shilingi bilioni 314.675 kwa maeneo ya taasisi na vijiji 38 katika Wilaya za Monduli, Arumeru na Manispaa ya Sindida yanaendelea na maeneo ya vijiji na taasisi hizo yatalipwa fidia kupitia Wakurugenzi wa Halmashauri husika ifikapo mwezi Juni, 2021.