Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 36 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 298 2021-05-25

Name

Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Primary Question

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali italeta Bungeni Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya Mkopo wa Elimu ya Juu ili kuwapunguzia mzigo mkubwa wa malipo wanufaika wa mkopo huo?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Khalifa Mohamed Issa, Mbunge Mtambwe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikifanya mapitio katika tozo na makato yanayohusu mikopo ya elimu ya juu ili kuwapunguzia mzigo wa tozo na makato wanufaika wa mikopo hiyo.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia maelekezo ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuanzia tarehe 01 Julai, 2021 Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, itafuta Tozo ya Asilimia Sita (6%) ya kulinda thamani ya fedha inayotozwa kwa wanufaika wa mikopo hiyo. Vilevile, Bodi ya Mikopo itatekeleza maelekezo yangu ya kuondoa tozo ya asilimia kumi (10%) ya wanufaika wanaochelewa kurejesha mkopo baada ya muda wa miezi 24 kupita baada ya kuhitimu.

Mheshimiwa Spika, kutokana na kupunguzwa kwa mzigo wa makato na tozo, nitoe wito kwa wanufaika wote wa mikopo ya elimu ya juu ambao hawajajitokeza, kuanza kurejesha mikopo hiyo ili fedha hizo ziwasomeshe Watanzania wengine wahitaji.