Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 37 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 314 2021-05-26

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE aliuliza:-

Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Umeme wa Maji kutoka Mto Rumakali katika Kata ya Lufilyo utaanza?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Atupele Fredy Mwakibete, Mbunge wa Busokelo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Umeme nchini (TANESCO) inatekeleza Mradi wa Kuzalisha Umeme kwa kutumia maporomoko ya maji ya Mto Rumakali, Mkoani Njombe.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu unahusu ujenzi wa kituo cha kuzalisha umeme cha megawati 222 na njia ya kusafirisha umeme msongo wa kilovoti 220 yenye urefu wa kilomita 150 kutoka Rumakali hadi Kituo cha Kupoza Umeme cha Iganjo, Mkoani Mbeya. Gharama za mradi ni takriban shilingi bilioni 913.

Mheshimiwa Naibu Spika, hatua iliyofikiwa sasa ni kukamilisha taratibu za manunuzi ya Mkandarasi wa ujenzi wa mradi. Kazi za ujenzi zinatarajiwa kuanza mwezi Oktoba, 2021 na kukamilika mwezi Juni, 2024.