Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 35 Water and Irrigation Wizara ya Maji 287 2021-05-24

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:-

(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kusambaza Maji kutoka katika mradi wa Maji Kata za
Miangalua na Mnokola katika Jimbo la Kwela?

(b) Je, ni lini Serikali itapeleka Pesa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi katika maeneo hayo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Kwela, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, hali ya upatikanaji wa maji katika Kata za Miangalua na Mnokola ni asilimia 51.2. Kata hizi ya Miangalua inapata huduma ya majisafi kupitia mradi wa Maji wa Skimu ya Miangalua ya visima virefu vinavyohudumia vijiji vya Miangalua, Tunko, Movu, Kavifuti na Nampako vya Kata hiyo na kijiji cha Mnokola kilichopo katika Kata ya Mnokola.

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha hali ya upatikanaji wa maji Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga inazidi kuimarika, Serikali imeendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maji ambapo kwa mwaka wa fedha 2020/ 2021 jumla ya miradi mitano ya maji imetekelezwa na kukamilika katika Vijiji vya Nankanga na Sakalilo (Kata ya Ilemba), Milepa na Kisa (Kata ya Milepa), Kizungu (Kata ya Muze) na miradi minne ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji katika Kata za Mtowisa, Ikozi, Msandamuungano na Mufinga.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/ 2022, Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 2.76 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi 18 ya maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga. Aidha, Serikali itatoa fedha kwa kuzingatia miongozo ya kupeleka fedha za utekelezaji wa miradi itakayopangwa katika bajeti husika.