Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 33 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 274 2021-05-21

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:-

Je, ni kwa nini Hospitali ya Mji Tarime isipandishwe hadhi na kuwa Hospitali ya Kanda Maalum ya Tarime na Rorya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Hospitali ya Mji Tarime ina Wodi nane na vitengo mbalimbali vya huduma ikiwemo maabara, jengo la mionzi, chumba cha upasuaji, huduma za mama na mtoto, chumba cha dawa, chumba cha magonjwa ya akili, macho, duka la dawa lakini pia miundombinu mingine. Hospitali hii inahudumia wastani wa wagonjwa 140 wa nje (OPD), lakini inahudumia wagonjwa 70 wanaolazwa kwa siku. Hospitali ina jumla ya vitanda 180.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kanda ya Ziwa tayari ina Hospitali ya Rufaa ambayo ni Hospitali ya Bugando iliyopo Mkoa wa Mwanza. Hivyo, Serikali haikusudii kuipandisha hadhi Hospitali ya Mji Tarime kuwa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Maalum ya Tarime na Rorya. (Makofi)