Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 31 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 271 2021-05-19

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:-

Je, Serikali ipo tayari kuanzisha Wilaya ya TANESCO kwa ajili ya kuhudumia viwanda na wananchi katika Mji wa Mafinga ili kuendana na kasi ya uchumi wa viwanda?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Mufindi ina Halmashauri mbili ambazo ni Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi na Halmashauri ya Mji wa Mafinga. Katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga, ipo Ofisi ya Wilaya ya TANESCO inayotoa huduma kwa wananchi wa Mji wa Mafinga pamoja na wananchi wa Wilaya ya Mufindi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa, Ofisi ya TANESCO iliyopo Mafinga inakidhi mahitaji ya kutoa huduma kwa wananchi wote wa Mji wa Mafinga ikiwa ni pamoja na wateja wa viwanda vikubwa 80, wateja wa viwanda vidogo vidogo 445 na wateja wadogo 23,207. Hata hivyo, Serikali kwa kutambua ukuaji wa shughuli za kiuchumi katika Mji wa Mafinga, TANESCO imefungua Ofisi Ndogo (Sub Office) katika Kata ya Igowelo, Kibao na Mgololo katika Kata ya Makungu. Ofisi hizi zimeanzishwa ili kusogeza huduma karibu kwa wananchi walio mbali na Mji wa Mafinga ikiwa ni pamoja na kuhakikisha huduma zinatolewa kwa urahisi kwa wananchi wa maeneo hayo.