Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 31 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 266 2021-05-19

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VUMA A. HOLLE K.n.y. MHE. SYLIVIA F. SIGULA aliuliza:-

Je, nini Mpango wa Serikali kuhakikisha kuwa Timu ya Taifa Stars inafanya vizuri katika Michezo ya Kimataifa?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sylvia Francis Sigula, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha kuwa Timu za Taifa ikiwemo Taifa Stars zinafanya vizuri katika mashindano mbalimbali, kuanzia mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali imeendelea kuboresha maandalizi ya timu zetu kwa kutenga fedha za kuzihudumia timu hizi. Mipango mingine iliyowekwa na Serikali ni ile ya muda mrefu na muda mfupi. Mipango ya muda mfupi ni pamoja na:-

(a) Kushirikiana na TFF katika maandalizi ya kambi za Timu ya Taifa ndani na nje ya nchi.

(b) Kuongeza motisha kwa kutoa posho na bonasi kwa wachezaji na benchi la ufundi la Timu ya Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mipango ya muda mrefu ni pamoja na:-

(a) Kuwekeza katika michezo ya UMITASHUMTA, UMISSETA.

(b) Kuanzisha Mfuko wa Maendeleo ya Michezo nchini.

(c) Mazungumzo yanaendelea kati ya Wizara yetu na Wizara ya Fedha ili kuhakikisha fedha hizi zinatengwa.

(d) Kuanzisha shule maalum za michezo katika kila mkoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mipango mingine ya Serikali iliyopo ni ushirikiano kati ya Wizara yangu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Ofisi ya TAMISEMI juu ya uendeshaji bora wa michezo nchini na mipango ya uanzishaji wa tahasusi za kidato cha Tano zenye somo la michezo.