Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 31 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 265 2021-05-19

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:-

Je ni lini Serikali itaweka vifaa vya maabara kwenye maabara zote za Shule za Sekondari katika Wilaya ya Mkalama zilizojengwa kwa nguvu za wananchi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Iramba Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama ina jumla ya shule 20 za Sekondari ambapo 19 kati ya hizo ni shule za Serikali. Usambazaji wa vifaa vya maabara mashuleni huzingatia ukamilishaji wa vyumba vya maabara katika shule husika. Hadi Machi, 2021, Serikali imepeleka vifaa vya maabara kwenye shule 18 kati ya shule 19 za sekondari katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, shule ya sekondari Kikhonda haijapelekewa vifaa kwa sababu haina vyumba vya maabara. Hata hivyo, Halmashauri kwa kushirikiana na wananchi wa Kata ya Kikhonda wameanza taratibu za ujenzi wa maabara katika shule hiyo ili ujenzi utakapokamilika iweze kuingizwa kwenye mpango wa kupatiwa vifaa.