Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 30 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 255 2021-05-18

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE K.n.y. MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza barabara za Singida Kaskazini zinazounganisha Vijiji ambazo hazipitiki kwa sasa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aysharose Mattembe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Singida Kaskazini ina mtandao wa barabara wenye urefu wa kilometa 811.68 ambao umekuwa ukifanyiwa matengenezo pamoja na kujenga na kukarabati vivuko. Katika mwaka wa fedha 2019/2020, TARURA Halmashauri ya Wilaya ya Singida ilifanya matengenezo ya barabara zenye urefu wa kilometa 78.55 na vivuko 22 kwa gharama ya shilingi milioni 739.39.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka fedha 2020/2021, barabara zenye urefu wa kilometa 67.8 na vivuko 20 vimetengenezwa kwa gharama ya shilingi millioni 711.08 ambapo hadi Machi, 2021 barabara zenye urefu wa kilomita 45 na vivuko 15 vimekamilika. Aidha, katika mwaka wa fedha 2021/2022 barabara zenye urefu wa kilomita 62.5 na vivuko 24 vitajengwa kwa gharama ya shilingi millioni 711.08.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini Halmashauri ya Wilaya ya Singida itafanya tathmini ya barabara zote za Singida Kaskazini ili kuandaa mpango wa namna bora ya kuweka vipaumbele vya ujenzi na matengenezo ya barabara.