Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 29 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 251 2021-05-17

Name

Augustine Vuma Holle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE K.n.y. MHE. VUMA A. HOLLE aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Barabara ya Kasulu - Uvinza kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Vuma Holle, Mbunge wa Kasulu Vijijini kama ifuatavyo;

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeanza ujenzi wa barabara ya Kasulu – Uvinza yenye urefu wa kilometa 65.9 kwa kiwango cha lami ambapo kilometa 8.9 kutoka Kasulu njiapanda ya Kanyani ni sehemu ya mradi wa barabara ya Kidakhawe – Kasulu yenye urefu wa kilometa 63 ambayo ujenzi wake kwa kiwango la lami umekamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, wakati Serikali inaendelea kutafuta fedha za ujenzi wa sehemu ya njia panda ya Kanyani hadi Uvinza, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali kila mwaka ili iweze kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka wa fedha wa 2020/2021 barabara hii imetengewa jumla ya shilingi milioni 1,887.9 kwa ajili ya matengenezo mbalimbali. Ahsante.