Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 29 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 250 2021-05-17

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza:-

Je, serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya huduma ya kipolisi katika maeneo ya pembezoni mwa miji ikiwemo na mkoa wa Dar es Salaam?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mara nyingine tena kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Elias Mahawanga Mbunge Wa Viti Maalum kutoka mkoa wa Dar es Salaam, kama ifuatavyo:

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi inatekeleza mpango wa Askari Polisi kata /shehia katika kata zote 3956 na shehia 335 za Tanzania, ambapo hadi kufikia mwezi Februari, 2021 jumla ya askari 3963 wameshapangwa kwenye kata/shehia zikiwemo kata zilizopo pembezoni mwa Mkoa wa Dar es Salaam na maeneo mengine kwa lengo la kutoa huduma za kipolisi pembezoni kuliko na idadi kubwa ya watu na huduma ya vituo vya polisi ipo mbali, lengo ni kushirikiana na wananchi katika ulinzi na kupunguza uhalifu katika jamii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa baadhi ya maeneo huduma za polisi ziko mbali, Jeshi la Polisi kupitia mpango wa askari kata limekuwa likishirikiana na walinzi wa jadi ikiwemo sungusungu ili kupambana na kutatua uhalifu huo. Nakushukuru.