Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 49 Education, Science,Technology and Vocational Training, Ofisi ya Rais TAMISEMI. 420 2016-06-23

Name

Dr. Elly Marko Macha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL (K.n.y. MHE. DKT. ELLY M. MACHA) aliuliza:-
Kufuatia Mpango wa Serikali wa utoaji wa elimu bure kuanzia Elimu ya Msingi hadi Sekondari na kwamba, watu wenye Ulemavu wanakabiliwa na umasikini uliokithiri na hivyo kushindwa kumudu gharama za elimu:-
(a) Je, Serikali iko tayari kutoa elimu bure kwa wanafunzi wenye ulemavu kwa ngazi ya Kidato cha Tano na Sita?
(b) Je, Serikali inaweza kulihakikishia Bunge hili kwamba itaweka utaratibu mzuri wa usafiri na huduma nyingine muhimu za kuwawezesha wanafunzi wenye ulemavu kupata elimu katika shule wanazopangiwa?
(c) Je, Serikali inaweza kulithibitishia Bunge hili kwamba wanafunzi wenye ulemavu wanaoingia Vyuo Vikuu watapewa kipaumbele katika kupata mikopo bila usumbufu wowote?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Elly Marco Macha, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, kufuatia Mpango wa Serikali wa Utoaji Elimu Bure kuanzia Elimu ya Msingi hadi Sekondari na kwamba, watu wenye ulemavu wanakabiliwa na umasikini, Ofisi ya TAMISEMI imeandaa Mpango wa Utoaji wa Elimu ya Msingi bila malipo ili kutekeleza Sera ya Elimu ya Mwaka 2014. Sera hiyo inaelekeza kwamba wanafunzi wote wa madarasa ya Awali, Msingi na Kidato cha Kwanza hadi cha Nne wanatakiwa kusoma bila kulipia ada wala michango ya aina yoyote. Lengo ni kuhakikisha kuwa kila mtoto wa Kitanzania mwenye umri wa kwenda shule, anapata fursa ya kupata elimu. Aidha, Sera ya Elimu Msingi Bila Malipo haijumuishi wanafunzi wa Kidato cha Tano na cha Sita. (Makofi)
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, Mamlaka za Serikali za Mitaa zimekuwa zikiingilia kati kwa kutoa misaada kwa watoto wenye mahitaji maalum pale inapojitokeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, natoa wito kwa Waheshimiwa Wabunge na Jamii kwa ujumla kuhakikisha kwamba jukumu la kuwatunza na kuwalea wanafunzi wenye ulemavu ni la kwetu sote.
(c) Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria Na. 9 iliyoanzisha Bodi ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu, inatamka bayana kuwa waombaji wanaotakiwa kupewa kipaumbele katika kupewa mikopo ni pamoja na wanafunzi wenye ulemavu. Aidha miongozo ya ukopeshaji ambayo hutolewa na Serikali kila mwaka imeendelea kutamka wazi kuwa wanafunzi wenye ulemavu ni kundi linalotakiwa kupewa kipaumbele katika mikopo.