Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 29 Water and Irrigation Wizara ya Maji 247 2021-05-17

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KUNTI Y. MAJALA aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua changamoto kubwa ya maji inayowakabili wananchi wa Mji wa Chemba?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, Kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kunti Yussuf Majala, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua changamoto ya huduma ya maji inayowakabili wananchi wa Mji wa Chemba ambapo kwa sasa hali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama ni chini ya asilimia 50. Katika kutatua changamoto ya huduma ya maji katika mji huo, Serikali ina mpango wa muda mfupi na mpango wa muda mrefu.

Mheshimiwa Naibu Spika katika mpango wa muda mfupi, kazi zilizopangwa kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji katika mji huo kwa mwaka wa fedha 2021/2022 ni pamoja na ujenzi wa matanki mawili ya kukusanya maji ya ukubwa wa lita 50,000, nyumba ya mitambo ya kusukuma maji, ununuzi na ufungaji wa pampu nne (4), ununuzi na ulazaji wa mabomba ya umbali wa kilometa 11.6. Kukamilika kwa kazi hizo kutaongeza uzalishaji wa maji kutoka wastani wa lita 50,000 kwa siku hadi lita 320,000 kwa siku.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, kwa mpango wa muda mrefu, Serikali ilipata mkopo kutoka Serikali ya India kupitia Benki ya Exim India jumla ya Dola za Marekani millioni 500 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi katika miji 28 nchini ukiwemo Mji wa Chemba. Maeneo yatakayonufaika katika utekelezaji wa Mradi huo ni pamoja na Paranga, Makamala, Kambi ya Nyasa, Gwandi, Chambalo na Chemba yenyewe. Ujenzi unatarajiwa kuanza wakati wowote katika mwaka huu wa fedha 2020/2021 na umepangwa kutekelezwa kwa miezi 24.