Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 29 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 245 2021-05-17

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA (K.n.y. MHE. CATHERINE V. MAGIGE) aliuliza:-

Je, Serikali haioni kuwa ni wakati muafaka wa kuongeza bajeti ya TARURA Wilayani Ngorongoro ili kukabiliana na uharibifu wa barabara uliotokana na mvua kubwa zilizonyesha msimu wa mwaka 2019 na 2020?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Catherine Valentine Magige, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kukabiliana na changamoto ya uharibifu wa miundombinu ya barabara inayotokana na mvua kubwa zilizonyesha msimu wa mwaka 2019 na 2020, Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro katika mwaka wa fedha 2019/2020, ulifanya matengenezo ya barabara zenye urefu wa kilomita 94.4, vivuko 15 na daraja moja kwa gharama ya shilingi bilioni 1.08. Aidha, hadi kufikia Aprili, 2021, Serikali imeipatia TARURA Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro shilingi milioni 917.64 kati ya shilingi bilioni 1.05 zilizotengwa katika mwaka wa fedha 2020/2021 kwa ajili ya matengenezo ya barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2019/2020 sambamba na matengenezo ya kawaida, Serikali iliipatia TARURA Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro shilingi milioni 276.68 kwa ajili ya matengenezo ya dharura katika barabara zilizoharibiwa na mvua. Barabara zilizotengenezwa ni pamoja na kipande chenye urefu wa kilomita 1.2 na makalavati manne katika barabara ya Oldonyowas - Ormania mpaka Pipaya, ujenzi wa makalavati manne na madrifti matano katika barabara ya Mdito – Digodigo – Oldonyosambu na matengenezo ya kipande chenye urefu wa kilomita 1.5 na drifti moja katika barabara za Ormania mpaka Oldonyorock.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 shilingi bilioni 1.04 zimetengwa kwa ajili ya matengenenezo ya barabara zenye urefu wa kilomita 105, mifereji yenye urefu wa kilomita 1.1 na makalavati 30. Serikali itaendelea kuongeza fedha zinazotengwa kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya barabara kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.