Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 28 Water and Irrigation Wizara ya Maji 242 2021-05-12

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza:-

(a) Je, ni lini Serikali itaimarisha na kuboresha miundombinu ya maji ya Mamlaka ya Maji Makonde ili Wananchi waweze kupata maji ya uhakika?

(b) Je, Serikali inachukua hatua gani za dharura kuboresha upatikanaji wa maji Newala Vijijini ambapo kwa sasa uzalishaji ni ujazo wa lita 6,700 tu kwa siku badala ya lita 23,741?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Salum Mtanda Mbunge wa Jimbo la Newala Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua changamoto ya uchakavu wa miundombinu ya maji ya Mamlaka ya Maji Makonde inayohudumiwa Wilaya za Newala, Tandahimba na Nanyamba.

Katika kutatua changamoto hiyo, Serikali imeendelea na ukarabati wa miundombinu ambapo katika mwaka huu wa fedha 2020/2021 kazi zinazofanyika ni kukarabati mitambo na mfumo wa umeme katika vituo vya kuzalishia na kusukuma maji. Utekelezaji wa kazi hizi unalenga kuongeza uzalishaji wa maji kutoka meta za ujazo 6,700 kwa siku hadi meta za ujazo 11,116 kwa siku, kazi inatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kupata suluhisho la kudumu la tatizo la maji katika maeneo hayo, Serikali kuanzia mwaka 2021/2022 imepanga kutekeleza kazi mbalimbali ikiwemo kuongeza idadi ya visima vya kuzalisha maji kutoka 6 hadi 12 kwenye Bonde la Mitema pamoja na kupanua miundombinu ya kusafirisha maji uchimbaji wa visima utaongeza uzalishaji wa maji kutoka meta za ujazo 11,116 hadi Meta za ujazo 23,741 kwa siku. Kukamilika kwa kazi hizo kutaboresha upatikanaji wa huduma ya maji kutoka asilimia 58 za sasa hadi asilimia 95.

Vilevile Wizara ya maji kupitia RUWASA katika mwaka wa fedha 2020/2021, imeendelea na utekelezaji wa miradi ya maji Mchemo na Chiule iliyotarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2021 na miradi ya maji Mtongwele, Miyuyu na Mnima inayotarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2021. Katika mwaka 2021/2022, Serikali imetenga kiasi cha Shilingi bilioni
1.95 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali katika Wilaya Newala Vijijini.

Mheshimiwa Naibu Spika, Katika mpango wa muda mrefu, Serikali ilipata mkopo kutoka Serikali ya India kupitia Benki ya Exim India jumla ya dola za Marekani Milioni 500 kwa ajili ya utekelezaji wa Miji 28 ukiwemo mradi wa Makonde; ambapo maeneo yatakayonufaika ni vijiji 155 vya Wilaya ya Newala. Ujenzi unatarajiwa kuanza wakati wowote katika mwaka wa fedha 2020/2021.