Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 27 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 231 2021-05-11

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA aliuliza:-

Umeme wa msongo mkubwa wa KV 400 toka Singida hadi Namanga umepita katika baadhi ya maeneo ya wazi na malisho ya mifugo 6 kwenye Vijiji vya Engikaret, Ranchi, Orbomba, Kimokouwa na Eorendeke; na fedha za fidia ilipendekezwa zitolewe kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo ya Vijiji husika pamoja na watu binafsi ambao umeme huo umepita kwenye makazi yao:-

Je, ni lini fedha hizo zitatolewa?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Steven Lemomo Kiruswa, Mbunge wa Longido, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la TANESCO inaendelea kukamilisha ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoti 400 kutoka Singida hadi Namanga. Lengo kuu la mradi huu ni kuimarisha umeme katika Gridi ya Taifa na kuunganisha Tanzania na nchi za Zambia na Kenya katika gridi ya umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mradi huu mwezi Septemba, 2020 Serikali kupitia TANESCO ililipa fidia jumla ya shilingi bilioni 11.33 kwa wananchi wapatao 645 katika Wilaya ya Longido ikiwamo Vijiji vya Engikaret, Ranchi, Orbomba, Kimokouwa na Eorendeke. Malipo hayo yamelipwa kama ifuatavyo; Kijiji cha Eorendeke jumla ya shilingi 439,780,320, Kijiji cha Kimokouwa jumla ya shilingi 165,564,000, Kijiji cha Orbomba jumla ya shilingi 343,662,080 na Kijiji cha ranchi jumla ya shilingi 720,754,200.

Mheshimiwa Spika, malipo ya fedha hizi yalifanyika kwa njia ya hundi kupitia Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido.