Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 27 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 230 2021-05-11

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaunganisha mfumo wa gesi asilia kwa ajili ya kupata nishati ya kukaangia samaki katika Soko la Feri Manispaa ya Mtwara Mikindani?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Issa Malapo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) inaendelea na kazi ya ujenzi wa miundombinu ya kusambaza gesi asilia katika mikoa mbalimbali nchini ukiwemo Mkoa wa Mtwara kwa ajili ya matumizi ya viwandani, majumbani na taasisi za umma na binafsi. Katika Mkoa wa Mtwara, mradi huu unahusisha ujenzi wa miundombinu ya kusambaza gesi asilia kwa njia za mabomba na vituo vya kuongeza mgandamizo wa gesi (Compressed Natural Gas (CNG) Stations).

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa miundombinu ya usambazaji wa gesi asilia katika Soko la Feri katika Manispaa ya Mtwara Mikindani upo katika hatua ya kukamilisha usanifu wa kina wa kihandisi, utakaofuatiwa na hatua ya kumpata mkandarasi wa ujenzi wa mradi huo. Kazi ya usanifu inatarajiwa kukamilika mwezi Agosti, 2021 na ujenzi kuanza Desemba, 2021 na kukamilika Juni, 2022. Gharama za mradi ni takribani shilingi bilioni 10.11.