Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 25 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 206 2021-05-07

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:-

Je, Serikai haioni umuhimu wa kuajiri Wafamasia angalau katika kila Kituo cha Afya nchini ili kuimarisha usimamizi na mtiririko wa upatikanaji dawa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Selemani Jumanne Zedi, Mbunge wa Jimbo la Bukene, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa ikama wa watumishi wa afya, Mfamasia anapaswa kuwepo katika ngazi ya Hospitali. Kwenye ngazi ya Vituo vya Afya na Zahanati, ikama inaelekeza kuwepo kwa Mteknolojia wa Dawa au Mteknolojia Msaidizi wa Dawa. Kada hizi ni muhimu kuwepo kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ili kuimarisha uratibu na usimamizi wa bidhaa za afya.

Mheshimiwa Spika, kuanzia Mei, 2017 hadi Februari, 2021 Ofisi ya Rais, TAMISEMI imeajiri Wafamasia 79, Wateknolojia wa Dawa 313 na Wateknolojia wa Dawa Wasaidizi 160. Serikali inatambua changamoto ya uhaba wa Wataalam hawa, ambapo katika mwaka wa fedha 2021/ 2022 imepanga kuajiri watumishi 10,467 wakiwemo Wafamasia na Wateknolojia wa Dawa watakaopelekwa kwenye Hospitali za Halmashauri, Vituo vya Afya pamoja na zahanati kote nchini.