Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 23 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 198 2021-05-05

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Handeni- Kiberashi-Kiteto – Mrijo – Chemba – Kwa mtoro hadi Singida kwa kiwango cha lami kwa kuwa ipo kwenye Ilani na pia Ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Lujua Monni, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Handeni – Kiberashi – Kwa mtoro – Singida ni barabara ya mkoa yenye urefu wa kilometa 461. Kati ya urefu huo, kilometa 111 zipo Mkoa wa Manyara, kilometa 171 Mkoa wa Dodoma na kilometa 47.1 Mkoa wa Singida. Barabara hii nikiunganisha muhimu cha Mikoa ya Singida, Manyara, Dodoma na Kanda ya Pwani hasa bandari ya Tanga na Dar es salaam. Kukamilika kwa barabara hii kutapunguza idadi ya magari ya nayopita katika barabara kuu ya kati Central Corridor kuelekea Kanda ya Kati na Kanda ya ziwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS), imekamilisha Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina wa barabara hii. Kwa sasa Serikali ipo katika maandalizi ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hii. Katika Mwaka wa Fedha 2021 jumla ya Shilingi bilioni 6 zimetengwa kwa ajili ya kuanza maandalizi ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Aidha, katika mapendekezo ya bajeti ya mwaka 2021/22 barabara hii itazingatiwa.