Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 22 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 186 2021-05-04

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Kata za Mwamalole, Mbushi, Mwamanongu, Imalaseko, Mwamanimba, Mwabuzo na Kimali ili wananchi waweze kufaidika na huduma hiyo na kuchochea maendeleo katika Kata hizo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Leah Jeremiah Komanya, Mbunge wa Meatu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mradi Kabambe wa kupeleka umeme vijijini unaosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea kupeleka umeme katika kata na vijiji vyote ambavyo havijafikiwa na umeme Tanzania Bara zikiwemo Kata za Mwamamole, Mwamanimba, Mwabuzo, Imalaseko, Mwamanongu, Mbushi na Kimali. Kata hizi pamoja na vijiji vyake vyote vya Meatu vinatarajiwa kufikishiwa umeme ifikapo mwezi Desemba, 2022.

Mheshimiwa Spika, kazi za mradi katika Wilaya ya Meatu zinajumuisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 555.90, msongo wa kilovoti 0.4 urefu wa kilomita 48, ufungaji wa transfoma 48 za 50kVA, pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 1,056. Gharama ya mradi huu ni takriban shilingi bilioni 22.6.