Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 22 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 185 2021-05-04

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika vijiji 127 vilivyobaki vya Mkoa wa Songwe?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juliana Daniel Shonza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Songwe una jumla ya vijiji 307 ambapo kati ya hivyo, vijiji 180 tayari vimeapatiwa umeme na vijiji 127 bado havijapatiwa umeme. Nia ya Serikali ni kuvipatia umeme vijiji vyote visivyo na umeme kabla ya mwisho wa mwaka 2022.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TANESCO na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea kupeleka umeme katika vijiji vyote ambavyo havijafikiwa na umeme Tanzania Bara. Vijiji 127 vilivyobaki katika Mkoa wa Songwe vitapatiwa umeme kupitia utekelezaji wa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili ambapo utekelezaji wake ulianza mwezi Machi, 2021 na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022.

Mheshimiwa Spika, kazi za mradi kwa Mkoa wa Songwe zinajumuisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 1,065.4, msongo wa kilovoti 0.4 urefu wa kilomita 120, ufungaji wa transfoma 120 za 50kVA, pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 2,640. Gharama ya mradi huu ni takriban shilingi bilioni 38.7.