Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 21 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 173 2021-05-03

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga Daraja la Mto Bubu ili wananchi wa upande wa pili wa mto waweze kuvuka na kupata huduma mbalimbali za kijamii?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Juma Makoa, Mbunge wa Kondoa Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Daraja la Mto Bubu lijulikanalo kama Munguri B lipo katika barabara ya Kondoa – Nunguri – Mtiriangwi – Gisambalang – Nangwa yenye jumla ya urefu wa kilomita 81.4. Barabara hii inaunganisha Mkoa wa Dodoma na Mkoa wa Manyara kupitia Wilaya za Kondoa na Hanang.

Mheshimiwa Spika, mvua kubwa zilizonyesha mwaka 2019/2020 zilisababisha Mto Bubu kutanuka na kufanya Daraja la Munguri B kutopitika wakati wa mvua. Kwa kutambua changamoto hii, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS) imetenga fedha katika bajeti ya mwaka wa fedha 2021 kwa ajili ya kufanya usanifu wa Daraja jipya katika Mto Bubu.

Mheshimiwa Spika, taratibu za ununuzi wa kumpata Mhandisi Mshauri zipo katika hatua za mwisho ambapo kazi hiyo inatarajiwa kuanza Juni, 2021. Aidha, katika mapendekezo ya bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022, daraja hili limetengewa shilingi bilioni sita kwa ajili ya kukamilisha kazi ya usanifu. Baada ya usanifu kukamilika, ujenzi wa daraja hili utaanza kulingana na upatikanaji wa fedha. Ahsante.