Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 21 Water and Irrigation Wizara ya Maji 171 2021-05-03

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza.

Je, ni lini mradi wa maji wa kutoka Nyamtukuza, Kakora, Kharumwa, Izunya, Kayenze hadi Bukwimba utakamilika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu.

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nassor Amar Hussein, Mbunge wa Nyangh’wale, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mradi wa Maji wa Nyamtukuza uliopo Wilaya ya Nyang’hwale unalenga kuhudumia Vijiji 12 vya Nyamtukuza, Kakora, Bugombela, Nyarubele, Kitongo, Ikatangala, Kharumwa, Busengwa, Izunya, Kayenze, Bukwimba na Igeka. Hadi mwezi Machi, 2021, vijiji vinane (8) vimepata maji. Vijiji vilivyopata maji ni Nyamtukuza, Kakora, Kitongo, Ikatangala, Kharumwa, Busengwa, Nyarubele na Bugombela vimeanza kupata huduma ya maji.

Mheshimiwa Spika, mradi umepangwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni, 2021 na vijiji vyote 12 vitapata huduma ya maji ambapo wananchi wapatao 51,500 watanufaika. (Makofi)