Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 19 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 162 2021-04-29

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO - K.n.y. MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza:-

Usambazaji wa umeme vijijini unapaswa kukamilika ifikapo Mwaka 2021/2022:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kuwa usambazaji wa umeme vijijini unakamilika kama ilivyopangwa?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu Mzamili Zodo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika la Umeme (TANESCO) inaendelea kutekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili. Utekelezaji wa mradi huu ulianza mwezi Machi, 2021 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Disemba, 2022. Mradi huu unalenga kufikisha umeme katika vijiji 1,974 ambavyo havijafikiwa na miundo mbinu ya umeme. Aidha, mradi huu pia, utafikisha umeme katika vitongoji 1,474.

Mradi huu utakapokamilika utafanya vijiji vyote 12,268 vya Tanzania Bara kufikiwa na miundo mbinu ya umeme na gharama ya mradi huu ni takribani shilingi 1,040,000,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuhakikisha kuwa mradi huu unakamilika kwa wakati, Serikali imeweka mikakati mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuongeza usimamizi, kupunguza wigo wa kazi za wakandarasi ili kurahisisha usimamizi, wakandarasi kulipwa kwa wakati na kuhakikisha vifaa vyote vinavyohusika vinapatikana nchini.