Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 20 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 165 2021-04-30

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza:-

Je, ni kwa nini Serikali haioni umuhimu wa kurekebisha mfumo wa elimu na kuingiza mbinu tete na stadi za maisha ili kuwajengea uwezo wa kiushindani vijana wanaohitimu na kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante; kwa niaba ya Waziri Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nusrat Shaaban Hanje, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuwawezesha wanafunzi kupata stadi mbalimbali zikiwemo stadi za maisha na mbinu tete ili kuwa na uwezo wa kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo suala la ajira na kiteknolojia.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali itafanya mapitio ya mitaala ya shule za msingi na sekondari ili kuingiza stadi mbalimbali kama vile stadi za maisha hususan stadi za karne ya 21 na mbinu tete. Stadi za karne ya 21 ni pamoja na fikra tunduizi, ubunifu, ushirikiano, uongozi na stadi za teknolojia ya habari na mawasiliano. Stadi na mbinu hizi zitasaidia kuwajengea vijana uwezo wa kiushindani katika soko la ajira. Ahsante.