Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 20 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 163 2021-04-30

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. ALOYCE A. KWEZI - K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:-


Je, Serikali imechukua hatua gani kukabiliana na upungufu wa walimu na madawati hasa baada ya elimu ya msingi na sekondari kuwa bure?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE.DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, na kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Emmanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kuajiri walimu wa shule za msingi na sekondari ambapo kuanzia mwaka fedha 2016/2017 hadi 2020/2021 walimu 33,684 na mafundi sanifu maabara 497 wameajiriwa. Aidha, Ofisi ya Rais-TAMISEMI kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia itaajiri walimu 6,000 ifikapo tarehe 30 Julai, 2021 ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kukabiliana na upungufu wa madawati katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imetenga shilingi bilioni 7.15 kwa ajili ya kutengeneza madawati 710,000 katika shule za msingi. Aidha, Serikali inaendelea kushirikiana na wadau wa maendeleo pamoja na wananchi katika kutatua changamoto ya madawati kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini.